Watumiaji wa API

Toleo:

S26|01

Ilisasishwa mara ya mwisho tarehe:

03/02/2026

Jedwali la yaliyomo

Hapa, utapata masharti na vigezo vinavyohusiana haswa na Watumiaji wetu wa API (“API Terms”). Masharti haya ya API yanapaswa kusomwa pamoja na Masharti ya Jumla kwa Wabia wa Biashara (“Masharti ya Jumla”). Maneno yoyote yaliyotolewa maana maalum katika Masharti haya ya API yatakuwa na maana ileile kama ilivyofafanuliwa katika Masharti ya Jumla.

1. Wajibu wa Watumiaji wa API

1.1. Kwa kuzingatia unakidhi kikamilifu na kuendelea kufuata Masharti haya ya API, tunakupa leseni ya muda, isiyo ya kipekee, isiyoweza kupewa kwa wengine, isiyoweza kuhamishwa, na inayoweza kufutwa ya kutumia API yetu ili kuendeleza, kujaribu, na kusaidia programu ya kompyuta, tovuti, au bidhaa unayounda au huduma unayotoa (“Aplikesheni”) na kuruhusu wateja wako kutumia muunganisho wako wa API ndani ya Aplikesheni yako.

1.2. Unakubali kuwa hautafanya yafuatayo:

1.2.1. Kutoa leseni yoyote ndogo ya haki (sublicense) inayoruhusiwa chini ya Masharti haya ya API;

1.2.2. Kutumia au kunakili API yetu isipokuwa katika hali zilizoruhusiwa waziwazi na Masharti haya ya API;

1.2.3. Kutumia API yetu kwa madhumuni yoyote yanayokiuka sheria au kanuni yoyote au haki za mtu yeyote, ikiwa ni pamoja na haki za miliki, haki za faragha, au haki za utu; au

1.2.4. Kutumia API yetu kwa njia yoyote isiyoendana na Masharti haya ya API.

1.3. API yetu ina mipaka ya matumizi ili kuzuia matumizi mabaya na/au matumizi yasiyo sahihi ya API yetu. Mipaka hii ya matumizi inaweza kubadilishwa bila kupewa taarifa. Ikiwa utazidi mara kwa mara kikomo cha matumizi au kutumia huduma vibaya kwa namna yoyote ile, tunaweza kuzuia upatikanaji wako wa API yetu.

 2. Hifadhi ya maudhui

2.1. Huruhusiwi kuhifadhi maudhui yoyote (kama vile mlisho wa data) yanayotokana au yanayoanzia kwenye tovuti yetu au yaliyopatikana kupitia API yetu.

2.2. Unaweza kuhifadhi ID za watumiaji za herufi na namba zinazotolewa mahsusi kwa Programu (API tokens) au tokeni za uthibitishaji zilizotolewa kupitia Open Authorisation Standard (OAuth tokens).

2.3. Unaweza kuhifadhi kwa muda (cache) maudhui yoyote yanayotoka kwenye tovuti yetu au yaliyopatikana kupitia API yetu kwa hadi saa ishirini na nne (24) tangu maombi ya maudhui hayo kufanywa kupitia API yetu.

 

2.4. Iwapo uhusiano wetu utasitishwa kwa sababu yoyote ile, lazima ufute kabisa maudhui yote yanayotokana au yanayoanzia kwenye tovuti yetu au yaliyopatikana kupitia API yetu, isipokuwa pale ambapo kufanya hivyo kungekusababishia kukiuka sheria yoyote inayotumika au wajibu uliowekewa na mamlaka ya serikali.

3. Umiliki

3.1. Mali yetu


3.1.1. Tunamiliki haki zote, hadhi, na maslahi yote, ikiwa ni pamoja na haki zote za mali miliki, katika API yetu na vipengele vyote, sehemu zote, na programu tekelezi za API yetu, na hatukupi haki yoyote, hadhi, au maslahi katika API yetu isipokuwa leseni iliyotolewa chini ya Masharti haya ya API.

3.1.2. Matumizi yako ya API yetu hayatakupa haki zozote za umiliki wa miliki ya kiakili zinazotuhusu sisi, au umiliki wa hadhi au maslahi yoyote katika haki hizo, ikiwemo haki zinazohusiana na majukwaa yetu ya biashara na tovuti yetu.

3.1.3. Hutapingana, wakati wowote, au kusaidia mhusika mwingine yeyote kupinga haki zetu za API yetu au mali nyingine yoyote ya miliki ya kiakili inayomilikiwa au kupewa leseni kwetu au washirika wetu.

3.1.4. Unakubali kuchukua hatua kama inavyotakiwa kwa njia ya haki ili kulinda haki zetu za API yetu.

3.1.5. Unakubali kwamba tunaweza kuendelea kufanya mabadiliko na maboresho kwenye API yetu, na kwamba tutamiliki mabadiliko na maboresho hayo. 

3.1.6. Hapa, unakabidhi na kuhamishia kwetu haki zako zote, umiliki, na maslahi yako yote kuhusu marekebisho au kazi zilizotokana na API yetu zilizoundwa na wewe au kwa niaba yako, bila kujali kama ziliundwa kwa kufata Masharti ya API. Uhamishaji huo unaanza kutumika mara tu marekebisho haya au kazi zinazozalishwa na hujumuisha haki zote chini ya sheria yoyote ya mali miliki, ikiwemo hakimiliki.

3.1.7. Hutachukua hatua yoyote ambayo inaweza kuhatarisha, kupunguza, au kushirikisha kwa njia yoyote ile mhusika mwingine katika umiliki wetu wa API yetu na haki zetu juu yake au kazi zozote zilizotokana nayo au masasisho yake.

3.1.8. Sehemu yoyote au mbinu za mfumo wowote au programu ya API inayotokana na API yetu au taratibu zetu za biashara, pamoja na haki yoyote, umiliki, au maslahi yanayohusiana, ikiwemo haki zote za mali miliki, zitakuwa mali yetu pekee.

3.2. Mali yako


3.2.1. Hatuidai umiliki wowote wa Aplikesheni yako isipokuwa kwa kiwango ambacho Aplikesheni yako inatumia API yetu.

3.2.2. Unatupatia haki isiyo na ada, isiyo ya kipekee, ya kimataifa, na isiyoweza kubatilishwa, chini ya haki zako zote za mali miliki, kufanya yafuatayo:


3.2.2.1. Kuchapisha jina lako na nembo yako (iwe na au bila kiunganishi kwa Aplikesheni yako) kwenye tovuti yetu, katika taarifa za vyombo vya habari, na katika nyenzo za matangazo bila ridhaa yako ya ziada;

3.2.2.2. Kutumia, kuonyesha, na kuendesha Aplikesheni yako pamoja na maudhui yake kwa madhumuni yoyote ya masoko au maonyesho;

3.2.2.3. Kufanya Aplikesheni yako ipatikane kwa wateja wetu; na

3.2.2.4. Kuelekeza wateja wetu kwenye Aplikesheni yako kwa kuiunganisha.

3.3. Michango kwa API yetu


3.3.1. Kwa kutuma mapendekezo au maoni mengine kuhusu API yetu kwetu (“Michango”), unakubali yafuatayo:


3.3.1.1. Hatutakuwa na wajibu wowote wa kudumisha usiri kuhusiana na Michango yako;

3.3.1.2. Tunaweza kutumia au kufichua (au kuchagua kutotumia au kutofichua) Michango hiyo kwa madhumuni yoyote, kwa njia yoyote, na kupitia vyombo vya habari vyovyote duniani kote;

3.3.1.3. Unatupa haki za kipekee na zisizoweza kubatilishwa za kutumia Michango yako kwa njia yoyote tutakayoitaka; na

3.3.1.4. Hauna haki ya kupata malipo au fidia ya aina yoyote kutoka kwetu chini ya hali zozote.

3.4. Marekebisho ya API yetu


3.4.1. Tunaweza kutoa matoleo mapya ya API yetu na kuhitaji utumie matoleo hayo mapya. Matumizi yako yanayoendelea ya API baada ya toleo jipya yatachukuliwa kama kukubali kwako mabadiliko hayo.

3.4.2. Utahitaji kuacha kutumia matoleo yote ya zamani ya API yetu ili kutumia matoleo yetu mapya ya API. 

3.4.3. Tunaweza kubadilisha, kusitisha, kukomesha, au kuondoa matumizi yoyote ya API yetu, ikiwemo upatikanaji wa huduma, taarifa, vipengele, au kazi yoyote inayoweza kufikiwa kupitia API yetu. Tutajitahidi kukujulisha kuhusu mabadiliko hayo, kusitishwa, kukomeshwa, au kuondolewa kwa huduma, kwa kutoa taarifa angalau siku saba (7) mapema kupitia njia zetu za Telegram na jukwaa la Vanilla.

3.4.4. Ingawa nia yetu ni kwamba API yetu iliyoboreshwa iwe sambamba na toleo la moja kwa moja lililotangulia la API yetu, hatutoi dhamana ya jambo hilo na hatutawajibika kwako kwa njia yoyote ile kwa kushindwa kwa API yetu iliyoboreshwa kuwa sambamba na toleo lolote la awali la API yetu.

4. Dhamana na vizingiti vya wajibu

4.1. Unadhibitisha kwamba una haki ya kutumia, kuzalisha, kusambaza, kunakili kuonyesha hadharani, kuendesha hadharani, na kusambaza Aplikesheni yako, isipokuwa maudhui yanayotokana au asili yake ni kutoka kwenye tovuti yetu au yanayopatikana kupitia API yetu.

4.2. Unatumia API yetu kwa hatari yako mwenyewe. Unachukua jukumu kamili na hatari ya hasara yoyote unayoweza kupata kutokana na kutumia au kupata API yetu.

4.3. Mbali na vizingiti vya wajibu vilivyoainishwa katika Masharti ya Jumla, tafadhali zingatia yafuatayo:


4.3.1. Hatutawajibika kwa aina yoyote ya hasara au uharibifu unaotokana na taarifa au bei kuchapishwa au kutolewa kupitia API yetu, au kutokana na makosa au mapungufu ya API yetu au yaliyomo ndani yake.

4.3.2. Hatutakuwa na uwajibikaji wowote unaotokana na maagizo, maamuzi ya uwekezaji, au ununuzi wa bidhaa au huduma za watu wengine (ikiwemo vyombo vya kifedha na sarafu) kulingana na taarifa zilizochapishwa au kutolewa kupitia API yetu.

5. Kanusho

5.1. Taarifa ya dhamana


5.1.1. Tunatoa API yetu kwa msingi wa ‘kama ilivyo’ na ‘inavyopatikana’ bila dhamana yoyote, iwe iliyo wazi au isiyo wazi, ya aina yoyote ile. Kwa kiwango kikubwa kinachoruhusiwa chini ya sheria inayotumika, tunakataa dhamana zote na uwakilishi wowote, ikiwemo bila kikomo dhamana yoyote isiyo wazi ya ubora wa bidhaa, kufaa kwa madhumuni maalum, umiliki, usahihi wa data, na kutokuvunja haki yoyote.

5.1.2. Hatutoi hakikisho kuwa API yetu itafanya kazi bila kuingiliwa au makosa yoyote. Kwa ujumla, uendeshaji wa API yetu unaweza kusitishwa kwa sababu mbalimbali ikiwemo matengenezo, masasisho, au kushindwa kwa mfumo au mtandao. Hatukubali uwajibikaji wowote kwa uharibifu wowote unaosababishwa na kusitishwa au makosa katika utendaji kazi.

5.1.3. Hatutakuwa na uwajibikaji wowote kwa matatizo yoyote ya utendaji, kutoweza kufikia, au hali mbaya ya matumizi ya API yetu kutokana na vifaa visivyofaa, matatizo yanayohusiana na watoa huduma za intaneti, matatizo ya mtandao wa intaneti, au sababu nyingine yoyote ile.

5.2. Taarifa ya usalama


5.2.1. Unakubali kwamba wewe pekee ndiye unayewajibika kwa udhibiti, uendeshaji, na usalama wa miamala na mawasiliano yoyote yanayofanyika kupitia ufikiaji au matumizi ya API yetu.

5.2.2. Kuna hatari zinazohusiana na kutumia mfumo wa utekelezaji wa biashara unaotegemea intaneti, ikiwemo kushindwa kwa vifaa, programu, na miunganisho ya intaneti. Hatudhibiti ubora wa mtandao, upokeaji wake au usambazaji wake kupitia intaneti, usanidi wa vifaa vyako, au uimara wa muunganisho wake. Hatutawajibika kwa kushindwa kwa mawasiliano, usumbufu, makosa, upotoshaji, au ucheleweshaji wowote utakaojitokeza unapofanya biashara kupitia intaneti kwa kutumia API yetu.

6. Fidia

6.1. Yafuatayo yatakuwa majukumu yako pekee, na utatulipa fidia na kutuweka huru na salama dhidi ya madai, uharibifu, au mashitaka yoyote ya wahusika wengine (ikiwemo hasara zozote za moja kwa moja au zisizo za moja kwa moja, upotevu wa faida, na gharama pamoja na matumizi yetu ya kisheria yanayokubalika ikiwa yatatumika) yanayotokana na yafuatayo:


6.1.1. Kushindwa kwako kudumisha usalama wa vifaa au taratibu zozote za usalama zinazotumika ndani au kuhusiana na API yetu;

6.1.2. Matumizi, uendeshaji, au mchanganyiko wa API, data, vifaa, au nyaraka vilivyo vyetu na vile visivyotuhusu vinavyosababisha uwajibikaji; na

6.1.3. Madai yoyote ya wahusika wengine yanayotokana na, au yanayohusiana na, matumizi yako ya, au kushindwa kwako kutumia, API yetu.

7. Ulinzi

7.1. Kama utagundua dosari zozote za usalama au uvunjaji wa usalama katika Aplikesheni yako, lazima utuarifu mara moja kwa kuanzisha mjadala kwenye Vanilla Community, ambayo ni sehemu ya tovuti yetu ya wasanidi programu, au kwa kutuma barua pepe kwenda api-support@ deriv.com

7.2. Utashirikiana nasi haraka kusahihisha dosari yoyote ya usalama na utaondoa mara moja uvunjaji wowote wa usalama au uvamizi.

7.3. Kama dosari yoyote ya usalama au uvunjaji wowote unaohusiana na Aplikesheni, API, au maudhui yaliyoko kwenye tovuti yetu au yanayopatikana kupitia API itatokea, hutatoa taarifa zozote kwa umma (ikiwemo kupitia vyombo vya habari, blogu, mitandao ya kijamii, bodi za matangazo, n. k.) bila idhini yetu ya wazi ya maandishi kabla ya tukio kila mara.

8. Usitishaji

8.1. Wakati wowote na kwa sababu yoyote au bila sababu yoyote, sisi, kwa maamuzi yetu pekee, tunaweza kusitisha matumizi yako ya API yetu bila taarifa yoyote.

8.2. Iwapo tutatekeleza haki yetu chini ya Kifungu cha 8.1, haki zote na leseni zilizoruhusiwa chini ya Masharti haya ya API zitasitishwa mara moja. Unakubali kuacha mara moja kutumia API yetu.